WATU wengi wanakabiliwa na changamoto ya namna ya kupanga nyumba kwa sababu ya kutozingatia vitu vidogo vichache, ambavyo vinaweza kuwafanya waifurahie sebule au chumba cha kulala.
1. Chunguza eneo linaloonekana zaidi
Kabla hujaanza kupanga kitu chochote katika sebule au chumba chako ni muhimu sana kuzingatia sehemu ambayo macho ‘yanapiga’ zaidi ili uweke kitu kitakachokufanya ufurahie unapoingia nyumbani kwako.
Eneo hili linaweza kujitengeneza lenyewe mathalani eneo lenye dirisha kubwa au usanifu mwingine wowote uliofanyika wakati wa ujenzi. Vinginevyo unaweza kulitengeneza kwa mfano eneo ambalo luninga na miziki itakaa. Popote pale penye eneo hili la kivutio ndipo unatakiwa upange fenicha kupazunguka.
2. Usigusishe kochi na ukuta
Ukubwa wa chumba au sebule, ndio unaamua ni eneo kiasi gani libaki ukutani bila kugusana na fenicha, ingawa hata kwenye sebule ndogo kabisa unapaswa kuacha
inchi kadhaa kati ya migongo ya fenicha na ukuta. Lakini kama una chumba kikubwa, panga fenicha katikati huku ukiacha hatua kadhaa kati ya fenicha na ukuta.
3. Tengeneza eneo la mazungumzo
Watu waliokaa sebuleni wanatakiwa waweze kuongea kawaida kwa uhuru bila kupayuka ama kuumiza shingo kumtazama anayeongea naye. Panga sofa na viti kwa mpangilio ambao zitatazama japo si kazima ziwe kwenye mstari ulionyooka bali ziwe karibukaribu. Kama sebule ni kubwa sana ni afadhali kuweka maeneo mawili. Wapo watu wenye sebule za hivi ambapo wana kawaida ya eneo moja kukaa wageni na la pili hukaa wenyeji.
4. Uwiano
Uwiano ni jambo muhimu sana kwenye kupanga fenicha sebuleni. Usipange kubwa tu peke yake na ndogo tu pele yake. Hakikisha unachanganya ukubwa na maumbo tofauti pamoja.
5. Zingatia pa kupita
Watu wasiruke kochi ili kupita. Kuwe na nafasi ya kutosha angalau hatua moja kati ya meza ya kahawa na sofa na pia viti.







Hakuna maoni:
Chapisha Maoni