KAMA kuna nguvu mbaya imeingia kwenye nyumba au maisha yako, maua au mimea itakuambia.
Mara nyingi yanatumia ishara, utayaona yanakauka au
yanachanua zaidi; wataalamu wanashauri kama unayo nyumbani au kazini kwako, ni
muhimu uamue kuwa rafiki yao.
Muhimu zaidi ni lazima uwe mcha Mungu na ukubali kuujaza
moyo wako upendo na uwe tayari kusamehe na kuondoa vinyongo.
Kama ni umasikini umeingia, utaona maua yako yanakauka
na kitaalamu, yapo maua yanayoweza kufukuza nguvu mbaya maishani mwako iwe ni
hali ya uchumi, mahusiano au maisha.
Miongoni mwa maua au mimea inayotoa ishara haraka ni ua pesa linalojulikana kama Money plant au Marble
queen Pothos, ambayo yanatajwa kuondoa nguvu ya umasikini.
Lingine ni ‘Peace Lily’ ambalo ni mahsusi kwa ajili ya
kuondoa huzuni na kukupa amani na Philodendron ambalo huongeza upendo na
kufukuza chuki.
Wataalamu wa mimea wanasema kwamba ukiona umeyahudumia vyema maua yako kwa kuyawekea mbolea, maji, mwanga na hewa na bado yaikafa, jichunguze
binafsi huenda upendo umeisha kwako au una mtu umembeba moyoni hujamsamehe.
“Ishara nyingine ni kwamba huenda una msongo wa mawazo
na hivyo hujipendi wewe mwenyewe au unayempenda hakupendi na wewe umeshindwa
kumpenda mtu mwingine…ukiona hivi panda ‘Philodendron’ ingia kwenye maombi na
utaona upendo ukija kwako,” anasema Anastazia Philemon, mtaalamu wa bustani.
Kwenye kipato anashauri kama una biashara au ofisi ni
muhimu kuweka ‘Money Plant’ na ikitokea imekufa, unapaswa kuingia kwenye maombi
mazito kuhusu uchumi wako.
“Hapo itabidi ufanye maombi ya ziada kwa ajili ya kazi
au biashara yako. Unaweza kupanda ua pesa lingine au mbadala kama ‘Marble Queen’
na utaona mambo yanabadilika. Maua yanakupa ishara za kiroho kwa hiyo ni vyema
ukajifunza kuwa mwombaji pia,” anasisitiza.
Kama unakosa furaha ya ndani na unaona maua yanadhohofu
tambua huzuni ipo malangoni pako. Wataalamu wanasema kuwa inawezekana kudhohofu
kwa maua yako ni kengele ya kukukumbusha kuomba kwa mzigo.
Ukiona ishara hii, ingia magotini na hakikisha
unaongeza ‘Peace Lily’ kwenye bustani yako na utaona hali inabadilika kwa kupata
amani na kuamsha maua yaliyokuwa yamesinzia.
Kama una msongo wa mawazo yaangalie maua yako utabaini
upo katika wakati gani nah atua unayopaswa kuchukua kwa sababu maua yanapenda
uwe na amani muda wote.
Maua hayapatani
na mtu asiye samehe, mtu mwenye vinyongo, ukiwa na maua nyumbani, kila unapopiga
hatua kwenye maisha yako usisahau kuyatazama maua.
Katika yote uyafanyayo, hakikisha unachukua hatua ya
maombi mapema, usije ukapanda tu maua ukamsahau Mungu, utafeli. Maua ni kama
mbwa anayebweka pale mtu asiye mwenyeji anapoingia ndani, yanakupa ishara ili
uchukue hatua ya kwenda mbele za Mungu.
PICHA ZOTE NA PINTEREST




Hakuna maoni:
Chapisha Maoni