Kwa mafundi na wataalamu wa ujenzi, ni rahisi zaidi kuchora ramani ya nyumba; na pale mtu anapotaka kufanya maboresho teknolojia imerahisisha ubunifu na kurahisha kazi. Unaweza kujiuliza inafanyaje kazi. Kwanza, unaweza kuipiga picha nyumba yako na kuiacha akili mnemba (AI), ‘ikushauri’ rangi ya kupaka, taa za nje au za ndani, jiko liweje na mpangilio wa kila chumba ufananeje.
Kama hiyo haitoshi, eneo la nje la wazi kuanzia kibaraza, iachie AI ikusaidie kukushauri, ili uweke samani na maua yatakayokupa hamasa ya kuishi nyumbani na kufurahia maisha. Mathalani, AI inaweza kukuambia ni wapi upande mti wa tunda gani, na uweke aina gani ya samani kama ni benchi na mwavuli au ujenge kibanda.
Kwenye kibaraza itakuambia aina ya maua utakayopanga na makopo yawe ya rangi gani pamoja na samani zake. Hata hivyo, inashauriwa kwamba baada ya kupata ushauri wa AI chukua uamuzi kulingana na uwezo wako na aina ya maua, miti ya matunda pamoja na samani unazoweza kuzipata kwa urahisi.
Anasema kwenye maliwato pamoja na kona, makabati hadi jikoni, AI haichoki kukupa ushauri; akisema zipo pia aplikesheni maalumu ambazo mtu anaweza kuzitumia kupata ushauri wa nini aweke wapi, nini apande kwenye bustani na eneo lipi libakie wazi.
PICHA ZOTE NA PINTEREST




Hakuna maoni:
Chapisha Maoni